Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

USHAMBULIAJI WA HOTEL YA ASASEY

Afrika - Chini ya Jangwa la Sahara

Tuzo

Up to $10 Million

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inatoa tuzo ya hadi milioni $10 kwa taarifa kuhusu mtu yeyote aliyehusika na shambulio la 2019 kwenye Hoteli ya Asasey huko Kismayo, Somalia.

Mnamo Julai 12, 2019, mshambuliaji wa kujitoa mhanga wa al-Shabaab alilipua kilipuzi kilichokuwa kimebebwa na gari katika Hoteli ya Asasey yenye geti, na kuruhusu magaidi wengine wa al-Shabaab kuingia kwenye kituo hicho. Washambuliaji hao waliwauwa watu 26 wakiwemo mmarekani mmoja na kuwajeruhi vibaya wengine 56. Vikosi vya usalama vya Somalia viliwaua washambuliaji wanne.

Al-Shabaab wanahusika na mashambulizi mengi ya kigaidi nchini Kenya, Somalia, na nchi jirani ambayo yameua maelfu ya watu, ikiwa ni pamoja na raia wa Marekani. Idara ya Nchi iliteua al-Shabaab kama Shirika la Kigeni la Kigaidi (FTO) na Kigaidi Maalumu cha Ulimwenguni (SDGT) mnamo Machi 2008. Aprili 2010, al-Shabaab pia iliteuliwa na Kamati ya Vikwazo ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ya Somalia kwa mujibu wa aya ya 8. ya azimio 1844 (2008).

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content