Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Tehrik-e Taliban Pakistani (TTP)

Asia Kusini na Kati

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tehrik-e Taliban Pakistan (TTP) ni kundi la kigaidi lenye makao yake nchini Pakistani na Afuganistani lililoanzishwa mnamo mwaka 2007. TTP inanuia kuisukuma serikali ya Pakistani kutoka Mkoa wa Khyber Pakhtunkwa (zamani ukijulikana kama Maeneo ya Kikabila Yaliyosimamiwa na Shirikisho) na kuanzisha utawala wa sharia kupitia vitendo vya kigaidi. TTP hupata mwongozo wa kiitikadi kutoka kwa al-Qa’ida (AQ), huku wanachama wa AQ wakiitegemea TTP kwa kiasi fulani maficho salama kwenye maeneo yaliyo karibu na mpaka kwa Afuganistani na Pakistani. Mpango huu umeipa TTP uwezo wa kuufikia mtandao wa kimataifa wa kigaidi wa AQ na ujuzi wa kiutendaji wa wanachama wake.

TTP imetekeleza na kudai kuhusika na vitendo vingi vya kigaidi dhidi ya maslahi ya Pakistani na Marekani, likiwamo shambulio la bomu la kujitoa mhanga la mwezi Disemba, mwaka 2009 kwenye kambi ya kijeshi ya Marekani, eneo la Khost, nchini Afuganistani ambalo liliwaua raia saba wa Marekani, na vilevile shambulio la bomu kujitoa mhanga mnamo mwezi Aprili, mwaka 2010 dhidi ya Ubalozi Mdogo wa Marekani eneo la Peshawar, Pakistani, ambalo liliwaua raia sita wa Pakistani. TTP inashukiwa kuhusika na mauaji ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Pakistan, Benazir Bhutto, mnamo mwaka 2007. TTP ilielekeza na kufadhili jaribio lililoshindikana la Faisal Shahzad kulipua kifaa kilipuzi katika eneo la Times Square jijini New York mnamo tarehe mosi, mwezi Mei, mwaka mwaka 2010.

Mnamo tarehe mosi, mwezi Septemba, mwaka 2010, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilitaja TTP kuwa Kundi la Kigaidi la Kigeni chini ya kifungu 219 cha Sheria ya Uhamiaji na Uraia, kama ilivyorekebishwa, na kama Gaidi wa Kimataifa Mwenye Sifa Maalumu kuambatana na Amri ya Rais 13224, kama ilivyorekebishwa. Matokeo yake ni kwamba, mali yote na maslahi ya TTP katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na TTP. Ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama ya kutoa, msaada wa nyenzo au rasilimali kwa TTP.

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content