Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Mtandao wa Fedha wa ISIS

Mashariki ya Karibu - Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati

Tuzo

Hadi dola milioni 10

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa zitakazowezesha kuvuruga taratibu za kifedha ya kundi la kigaidi la Dola la Kiislamu la Iraki na Siria (ISIS). ISIS inategemea ufadhili na kuwezesha mitandao kuendeleza operesheni na kuanzisha mashambulizi nchini Syria na eneo zinazojirani.

Mitandao ya ISIS imefanya uhamisho wa fedha ili kusaidia juhudi za ISIS nchini Syria katika kambi za watu waliokimbia makaazi yao kwa kukusanya fedha nchini Indonesia na Uturuki, baadhi ambazo zilitumika kulipa wanaosafirisha watoto nje ya kambi na kuwapeleka kwa wapiganaji wa kigeni wa ISIS kama wanaoweza kuajiriwa.

Wanaohurumia ISIS katika zaidi ya nchi 40 wametuma pesa kwa watu wanaohusishwa na ISIS katika kambi hizi ili kuunga mkono ufufuo tena wa ISIS siku zijazo.Katika al-Hawi – ikiwa na takriban watu 70,000, kambi kubwa zaidi ya wakimbizi hao kaskazini-mashariki nchini ya Syria – wafuasi wa ISIS wamepokea hadi dola 20,000 kwa mwezi kupitia hawala, utaratibu wa uhamisho usio wa rasmi; nyingi ya uhamisho huo wa kifedha, umetoka nje ya nchi ya Syria au kupitia nchi jirani kama vile Uturuki.

Shughuli haramu za kuuza mafuta, ulanguzi wa vitu vya kale vilivyoporwa kutoka Siria na Iraki pia ni vyanzo muhimu ambavyo huleta pesa taslimu na kuwezesha ISIS kutekeleza mbinu zake za kinyama na kuwadhulumu raia wasio na hatia. Uharibifu na uporaji wa maeneo ya kihistoria unaofanywa na ISIS nchini Siria na Iraki umeharibu ushahidi usioweza kubadilishwa wa maisha ya kale na jamii.

Sarafu za kale na za kihistoria, vito vya thamani, mawe ya thamani yaliyochongwa, sanamu, medali za ukumbusho, na mawe yenye maadishi ya kale ni miongoni mwa vitu vya kitamaduni ambavyo ISIS imelangua. Kwa msaada kutoka Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani, Baraza la Kimataifa la Majumba ya Makumbusho lilianzisha Orodha Nyekundu za Dharura za Vitu vya Kitamaduni vilivyo Hatarini ili kuwasilisha aina za vitu vya kitamaduni vilivyoporwa na kulanguliwa kutoka Siria na Iraki. Zinaweza kutazamwa hapa na hapa.

Picha:

Mahali Kunakohusiana:

Indonesia, Iraki, Siria, Uturuki

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content