Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Mitandao ya Utekaji Nyara ya ISIS (Wahubiri)

Mashariki ya Karibu - Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati

Tuzo

Hadi dola milioni 5

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu mitandao ya utekaji nyara ya ISIS au kwa taarifa zitakazowezesha kutambuliwa waliko, kuokolewa, na kurejeshwa kwa Maher Mahfouz, Michael Kayyal, Gregorios Ibrahim, Bolous Yazigi, na Paolo Dall’Oglio.

Mnamo tarehe 9 mwezi Februari, mwaka 2013, kasisi wa kanisa la Othodoksi la Ugiriki Maher Mahfouz na kasisi wa kanisa Katoliki la Armenia Michael Kayyal walikuwa ndani ya basi la umma wakisafiri kuelekea makao ya watawa na makasisi eneo la Kafrun, nchini Siria. Takribani kilometa 30 nje ya Aleppo, Siria, watu wanaoshukiwa kuwa wanachama wa ISIS wenye itikadi kali walisimamisha gari hilo, wakakagua hati za abiria, halafu wakawatoa Mahfouz na Kayyal kutoka kwenye basi hilo. Hawajaonekana wala kusikika tangu wakati huo.

Mnamo tarehe 22 mwezi Aprili, mwaka 2013, Askofu Mkuu wa kanisa la Othodoksi la Siria Gregorios Ibrahim alisafiri kutoka Aleppo hadi Uturuki kumchukua Askofu Mkuu wa kanisa la Othodoksi la Ugiriki Bolous Yazigi. Walipofika kwenye kituo cha ukaguzi wa magari barabarani karibu na al-Mansoura, nchini Siria, wanaume kadha waliokuwa na bunduki waliwavizia maaskofu hao na kutwaa gari lao. Dereva wa wahubiri hao alipatikana baadaye akiwa mfu. Maaskofu hao wanaaminika kuwa walitekwa nyara na watu walio na ushirika na al-Nusra Front, kundi mshirika wa al-Qa’ida;hata hivyo, maaskofu hao baadaye walihamishiwa kwa ISIS.

Mnamo tarehe 29 mwezi Julai, mwaka 2013, ISIS ilimteka nyara kasisi wa dhehebu la Jesuit la Italia Paolo Dall’Oglio kwenye eneo la Raqqah, nchini Siria. Padre Dall’Oglio alikuwa amepanga kukutana na ISIS ili kuomba kuachiliwa huru kwa Mahfouz, Kayyal, Ibrahim, na Yazigi. Hajaonekana wala kusikika tangu wakati huo.

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content