Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Kundi la Al-Nusrah Front (ANF)

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Qa’ida nchini Iraq (AQI) Abu Bakr al-Baghdadi alimtuma kiongozi wa ANF Muhammad al-Jawlani nchini Syria kupanga vikundi vidogo vya kigaidi. Mnamo mwezi Aprili, mwaka 2013, al-Jawlani aliapa kutii kiongozi wa AQ Ayman al-Zawahiri. ANF ilijitenga kutoka AQI na kuwa kundi huru. Mnamo mwezi Januari, mwaka 2017, ANF iliungana na makundi mengine ya upinzani yenye siasa kali kuunda Hayat Tahrir al-Sham (HTS). ANF inasalia kuwa mshirika wa al-Qa’ida nchini Syria.

Lengo la ANF ni kuuondoa utawala wa rais wa Syria, Assad, na badala yake kuweka taifa la Kiislamu la dhehebu la Sunni. ANF ipo kwa wingi na inadhibiti sehemu ya eneo kaskazini magharibi mwa Syria, ambapo inaendeleza shughuli zake kama kundi la upinzani, na lina ushawishi wa viwango tofauti juu ya utawala wa ndani na njama za nje. ANF imetekeleza mashambulio kadha ya kigaidi kote nchini Syria, mara nyingi ikilenga raia.

Mnamo tarehe 15, mwezi Mei, mwaka 2014, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilitaja ANF kuwa Kundi la Kigaidi la Kigeni chini ya kifungu 219 cha Sheria ya Uhamiaji na Uraia, kama ilivyorekebishwa. Awali, mnamo tarehe 14 mwezi Mei mwaka 2014, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje iliitaja ANF kuwa Shirika la Kigaidi la Kigeni Lenye Sifa Maalumu kuambatana na Amri ya Rais 13224, kama ilivyorekebishwa. Kutokana na kutajwa huku, mali yote na maslahi ya ANF katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na ANF. Ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama kutoa ufadhili wa nyenzo au rasilimali kwa ANF.

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content