Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Jama’at Nusrat al-Islam wal-Muslimin (JNIM)

Afrika - Chini ya Jangwa la Sahara

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Jama’at Nusrat al-Islam wal-Muslimin (JNIM) limejieleza kama tawi rasmi la al-Qa’ida nchini Mali. Mnamo mwaka 2017, tawi la Sahara la al-Qa’ida kwenye eneo la Kiislamu la Maghreb, al-Murabitoun, Ansar al-Dine, na Macina Liberation Front wote waliungana kuunda JNIM. Likiendesha shughuli zake nchini Mali, Nijeri, na Bukinafaso, JNIM limehusika na mashambulio mengi na utekaji nyara. Mnamo mwezi Juni, mwaka 2017, JNIM ilishambulia eneo maalum la mapumziko ya kitalii nje ya jiji la Bamako lenye kutembelewa sana na watu kutoka mataifa ya Magharibi na ilihusika na mashambulio makubwa yaliyoratibiwa jijini Ouagadougou mnamo tarehe 2 mwezi Machi, mwaka 2018. Mnamo mwezi Septemba, JNIM ililipua bomu la ardhini chini ya basi la abiria katikati mwa nchi ya Mali, likawaua raia 14 na kuwajeruhi wengine 24.

Mnamo tarehe 6 mwezi Septemba, mwaka 2018, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilitaja JNIM kuwa Kundi la Kigaidi la Kigenii chini ya kifungu 219 cha Sheria ya Uhamiaji na Uraia, kama ilivyorekebishwa. Hapo awali, mnamo tarehe 5 mwezi Septemba, mwaka 2018, Wizara ya Mambo ya Nje iliitaja JNIM kuwa Gaidi wa Kimataifa Mwenye Sifa Maalumu kuambatana na Amri ya Rais 13224, kama ilivyorekebishwa. Matokeo yake ni kwamba, mali yote na maslahi ya JNIM katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na JNIM. Ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama ya kutoa, msaada wa nyenzo au rasilimali kwa JNIM.

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content