Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Hafiz Saeed

Asia Kusini na Kati

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni kumi kwa taarifa kumhusu Hafiz Saeed, mwanzilishi na kiongozi wa Lashkar-e-Tayyiba (LeT), kundi lililotajwa na Marekani kama Shirika la Kigaidi la Kigeni (FTO). Saeed alishiriki katika kupanga shambulio la kigaidi kwa siku nne dhidi ya mji wa Mumbai, India mnamo mwezi Novemba, mwaka 2008 ambapo watu 166 waliuliwa, wakiwamo Wamarekani sita.

Mnamo mwaka 2020, mahakama ya kupambana na ugaidi ya Pakistani ilimpata Saeed na hatia kwa makosa mbalimbali ya kufadhili ugaidi na ikamhukumu kufungwa gerezani. Marekani inaendelea kutafuta taarifa kumhusu Saeed kwa sababu mfumo wa mahakama wa Pakistan umewaachilia huru viongozi na majasusi wa LeT waliopatwa na hatia hapo awali.

Mnamo tarehe 27 mwezi Mei, mwaka 2008, Wizara ya Fedha ya Marekani ilimtaja Saeed kama Gaidi wa Kimataifa Mwenye Sifa Maalumu kuambatana na Amri ya Rais 13224, kama ilivyorekebishwa. Matokeo ya kutajwa huku, miongoni mwa matokeo mengine, ni kwamba mali yote na maslahi ya Saeed katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na Saeed. Aidha, ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama ya kutoa, msaada wa nyenzo au rasilimali kwa FTO LeT. Mnamo tarehe 10 mwezi Disemba, mwaka 2008, Saeed aliorodheshwa kwenye Kamati ya Umoja wa Mataifa 1267/1989 ya Vikwazo vya al-Qa’ida kama mtu anayehusishwa na shirika la kigaidi la al-Qa’ida na, hivyo basi, yuko chini ya vikwazo vya kimataifa.

Picha:

Mahali Kunakohusiana:

Pakistan

Tarehe ya Kuzaliwa:

Mnamo tarehe 5, mwezi Juni, mwaka 1950

Mahali pa Kuzaliwa:

Sargodha, Punjab, Pakistani

Uraia:

Pakistani

Utaifa:

Pakistani

Nambari ya (za) Paspoti na Nchi:

Kijitabu A5250088 (Pakistani); BE5978421 (Pakistani);

Nambari ya (za) Utambulisho wa Kitaifa na Nchi:

23250460642 (Pakistani); 3520025509842-7 (Pakistani)

Jinsia:

Mwanamume

Rangi ya Nywele:

Nyekundu

Rangi ya Macho:

Kahawia

Lakabu/Tahajia Mbadala za Majina:

Muhammad Saeed; Hafiz Muhammad Saeed; Hafez Mohammad Sayeed; Hafiz Mohammad Saeed; Hafiz Mohammad Sayid; Hafiz Mohammad Syeed; Hafiz Mohammad Sayed; Muhammad Saeed Hafiz; Hafiz Sahib; Tata Ji

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content