Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Al-Qa’ida katika eneo la Kiislamu la Maghreb (AQIM)

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Mwanzoni likijulikana kama Kundi la Kisalafi la Mahubiri na Vita, al-Qa’ida (GSPC) katika eneo la Kiislamu la Maghreb (AQIM) ilitokea baada ya kundi hilo kuahidi utii kwa al-Qa’ida mnamo mwaka 2006. Ingawa kwa kiasi kikubwa AQIM lingali kundi la kigaidi linaloendesha shughuli zake kwenye eneo la Sahel, limechukua matamshi na itikadi kali zaidi dhidi ya mataifa ya Magharibi.

Mara kwa mara AQIM imefanya vitendo vya ugaidi, ikiwemo mabomu ya kujitoa mhanga, kuwashambulia raia, na harakati za utekaji nyara kwa ajili ya fidia. Shambulio la bomu lililofanywa na AQIM mnamo mwaka 2007 dhidi ya jengo la makao makuu ya Umoja wa Mataifa na jengo la serikali ya Aljeria jijini Algiers liliwaua watu 60. Mnamo mwezi Januari mwaka 2016, AQIM ilishambulia hoteli moja nchini Bukinafaso ambalo liliwaua watu 28 na kuwajeruhi 56. Mnamo mwezi Machi, mwaka 2016, AQIM ilidai kuhusika na shambulio dhidi ya eneo maalum la mapumziko ya kitalii ufukweni Kodivaa ambalo liliwaua watu 16 na kuwajeruhi wengine 33. Mnamo Januari mwaka 2017, AQIM ilitekeleza shambulio la kujitoa mhanga ambalo liliwaua watu zaidi ya 50 mjini Gao, Mali.

Mnamo tarehe 27, mwezi Machi, mwaka 2002, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilitaja AQIM kuwa Kundi la Kigaidi la Kigeni chini ya kifungu 219 cha Sheria ya Uhamiaji na Uraia, kama ilivyorekebishwa. Hapo awali, mnamo tarehe 23, mwezi Septemba, mwaka 2001, AQIM iliorodheshwa kwenye Kiambatanisho cha cha Amri ya Rais 13224, na kutokana na hiyo, inakabiliwa na vikwazo chini ya Amri hiyo kama Gaidi wa Kimataifa Mwenye Sifa Maalumu. Matokeo yake ni kwamba, mali yote na maslahi ya AQIM katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na AQIM. Ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama ya kutoa, msaada wa nyenzo au rasilimali kwa AQIM.

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Signal app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Telegram app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Signal ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Telegram ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content