Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Al-Qa’ida (AQ)

Mashariki ya Karibu - Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Al-Qa‘ida (AQ) ilipangwa na Usama bin Ladin mnamo mwaka 1988 ikiwa na Waarabu waliopigana nchini Afuganistani dhidi ya vikosi vya kijeshi vilviyoikalia nchi hiyo vya Muungano wa Kisovieti uliovunjika sasa. AQ hujitahidi kuondoa ushawishi wa Ulaya Magharibi kutoka mataifa ya Kiislamu, kupindua serikali za ‘uasi’ za mataifa ya Kiislamu, na kuanzisha ukhalifa wa Kiislamu unaotawaliwa kwa ufasiri wa AQ wa sharia na ambayo hatimaye itakuwa kitovu katika mpangilio mpya wa kimataifa. Kimsingi malengo haya hayajabadilishwa tangu kundi hilo litangaze vita hadharani dhidi ya Marekani. AQ imepoteza majasusi wengi wa viwango vya kadiri na vya juu kutotana na juhudi za kukabiliana na ugaidi, lakini inaendelea kusajili, kupanga, kuhimiza, na kutekeleza mashambulio. AQ ina mashirika inayoshirikiana nayo katika maeneo ya Mashariki ya Kati, Afrika, na Asia na nguvu zake kwa sasa kimsingi zipo kwenye makundi-shirika hayo.

AQ imehusika na mashambulio mengi makubwa na yenye majeruhi wengi. AQ ilitekeleza mashambulio matatu ya mabomu dhidi ya wanajeshi wa Marekani kwenye eneo la Aden, nchini Yemen mnamo mwaka 1992 na ikadai kuangusha kwa makombora helikopta za Marekani na kuwaua wanajeshi wa Marekani nchini Somalia mnamo mwaka 1993. AQ pia ilitekeleza mashambulio ya mabomu mnamo mwaka 1998 dhidi ya Balozi za Marekani mijini Nairobi na Dar es Salaam yaliyowaua watu 224 na kuwarejuhi wengine zaidi ya 5,000. Mnamo mwezi Oktoba mwaka 2000, AQ ilitekeleza shambulio la kujitoa mhanga dhidi ya meli ya USS Cole kwenye bandari ya Aden kwa kutumia boti iliyojazwa vilipuzi, shambulio ambalo liliua mabaharia 17 wa Jeshi la Majini la Marekani na kujeruhi zaidi ya 30. Mnamo mwezi Septemba 11 mwaka 2001, wanachama 19 wa AQ waliteka na kuangusha ndege nne za abiria za Kimarekani – mbili kwenye jumba la World Trade Center jijini New York, moja Pentagon, na ya mwisho kwenye shamba lililo katika eneo la Shanksville, Pennsylvania. Mashambulio hayo ya 9/11 yaliua karibu watu 3,000.

Mnamo tarehe 8 mwezi Oktoba, mwaka 1999, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marerkani ilitaja AQ kuwa Kundi la Kigaidi la Kigeni chini ya kifungu 219 cha Sheria ya Uhamiaji na Uraia, kama ilivyorekebishwa. Mnamo tarehe 23 mwezi Septemba, mwaka 2001, AQ iliorodheshwa kwenye Kiambatanisho cha Amri ya Rais 13224. Kutokana na kutajwa huku, miongoni mwa matokeo mengine, mali yote na maslahi ya AQ katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na AQ. Aidha, ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama ya kutoa msaada wa nyenzo au rasilimali kwa AQ.

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content