Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Abu Ubaydah Yusuf al-Anabi

Afrika - Chini ya Jangwa la Sahara | Mashariki ya Karibu - Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati

Tuzo

Hadi dola milioni 7

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni saba kwa taarifa kumhusu Abu Ubaydah Yusuf al-Anabi, anayejulikana pia kama Abou Obeida Youssef al-Annabi na Yazid Mubarak. Al-Anabi ni kiongozi wa shirika la kigaidi la al-Qa’ida Kwenye Maghreb ya Kiislamu (AQIM). AQIM lilimtangaza al-Anabi kama kiongozi wake mpya mnamo mwezi Novemba, mwaka 2020. Al-Anabi aliahidi utii kwa kiongozi wa al-Qa’ida (AQ) Ayman al-Zawahiri kwa niaba ya AQIM’s na anatarajiwa kushiriki katika usimamizi wa kimataifa wa AQ.

Al-Anabi, ambaye ni raia wa Aljeria, awali alikuwa kiongozi wa Baraza la Watu Mashuhuri la AQIM na alitumika katika Baraza la Shura la AQIM. Al-Anabi alikuwa hapo zamani mkuu wa vyombo vya habari wa AQIM.

Mnamo tarehe 9 mwezi Septemba, mwaka 2015, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilimtaja al-Anabi kuwa Gaidi wa Kimataifa Mwenye Sifa Maalumu kuambatana na Amri ya Rais 13224, kama ilivyorekebishwa. Matokeo ya kutajwa huku, miongoni mwa matokeo mengine, ni kwamba mali yote na maslahi ya al-Anabi katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na al-Anabi. Aidha, ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama ya kutoa, msaada wa nyenzo au rasilimali kwa AQIM, kundi lililotajwa na Marekani kama Shirika la Kigaidi la Kigeni. Al-Anabi aliwekwa kwenye orodha ya vikwazo ya Azimio 1267 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSCR 1267) mnamo tarehe 29 mwezi Februari, mwaka 2016, hivyo kumfanya kukabiliwa na uwezekano wa mali yake kudhibitiwa kimataifa, kupigwa marufuku ya kusafiri, na vikwazo vya silaha.

Picha:

Mabango

Mahali Kunakohusiana:

Aljeria, Mali

Tarehe ya Kuzaliwa:

Mnamo tarehe mosi, mwezi Januari, mwaka 1969;mnamo tarehe 7, mwezi Februari, mwaka 1969

Mahali pa Kuzaliwa:

Annaba, Aljeria

Uraia:

Aljeria

Jinsia:

Mwanamume

Lakabu/Tahajia Mbadala za Majina:

Yusuf Abu-‘Ubaydah Al-Anabi;Abou Obeida Youssef Al-Annabi;Abu-Ubaydah Yusuf Al-Inabi;Mebrak Yazid;Youcef Abu Obeida;Mibrak Yazid;Yousif Abu Obayda Yazid;Yazid Mebrak;Yazid Mabrak;Yusuf Abu Ubaydah;Abou Youcef;Yazid Mubarak;Abu Ubaydah;Yusuf Abou Youcef

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content