Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Abu Ubaidah (Diriye)

Afrika - Chini ya Jangwa la Sahara

Tuzo

Up to $10 million

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni 10 kwa taarifa kumhusu Ahmed Diriye, anayejulikana pia kama Ahmed Umar na Abu Ubaidah. Abu Ubaidah anahudumu kama kiongozi wa al-Shabaab — nafasi ambayo ameishikilia tangu kifo cha kiongozi wa zamani wa al-Shabaab Ahmed Abdi Godane. Abu Ubaidah alikuwa mmoja wa wandani wa Godane wakati wa kifo cha Godane.

Kabla ya kuchukua nafasi ya Godane, Abu Ubaidah alitumika katika nyadhifa tofauti ndani ya al-Shabaab, zikiwamo kama msaidizi wa Godane, naibu gavana wa eneo la Lower Juba la Somalia mnamo mwaka 2008, na gavana wa al-Shabaab maeneo ya Bay na Bakool ya Somalia mnamo mwaka 2009. Kufikia mwaka 2013, alikuwa mshauri mwandamizi wa Godane, na alitumika katika “Idara ya Ndani” ya al-Shabaab, ambapo alisimamia shughuli za ndani za kundi hilo. Anashiriki maono ya Godane kwa mashambulio ya kigaidi ya al-Shabaab nchini Somalia kama kipengele cha matamanio makubwa ya kimataifa ya al-Qa’ida.

Mnamo tarehe 21 mwezi Aprili, mwaka 2015, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilimtaja Ubaidah kuwa Gaidi wa Kimataifa Mwenye Sifa Maalumu kuambatana na Amri ya Rais 13224, kama ilivyorekebishwa. Matokeo ya kutajwa huku, miongoni mwa matokeo mengine, ni kwamba mali yote na maslahi ya Ubaidah katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na Ubaidah. Aidha, ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama ya kutoa, msaada wa nyenzo au rasilimali kwa al-Shabaab, kundi lililotajwa na Marekani kama Shirika la Kigaidi la Kigeni.

Picha:

Mabango

Mahali Kunakohusiana:

Somalia

Tarehe ya Kuzaliwa:

1972

Mahali pa Kuzaliwa:

Somalia

Jinsia:

Mwanamume

Lakabu/Tahajia Mbadala za Majina:

Ahmed Diriye;Ahmad Umar Abu Ubaidah;Mahad Diriye;Ahmed Omar Abu Ubaidah;Sheikh Ahmad Umar Abu Ubaidah;Sheikh Ahmed Umar Abu Ubaidah;Sheikh Omar Abu Ubaidaha;Sheikh Ahmed Umar;Sheikh Mahad Omar Abdikarim;Ahmad Umar;Abu Diriye

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content