Tovuti rasmi ya serikali ya Marekani

Kuhusu

Muhtasari wa Programu

Historia ya Programu na Mamlaka za Kisheria

TKM, programu ya tuzo kwa usalama wa kitaifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, ilianzishwa mwaka 1984 na Sheria ya Kukabiliana na Ugaidi wa Kimataifa, Sheria ya Umma 98-533 (iliyopangwa wazi katika 22 U.S.C. § 2708). Chini ya usimamizi wa Ofisi ya Usalama wa Kidiplomasia ya Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje, dhamira ya TKM ni kutoa tuzo ili kupata taarifa inayolinda maisha ya Wamarekani na maslahi ya Marekani na kuendeleza usalama wa kitaifa wa Marekani.

Tangu 1984, Kongamano imepanua mamlaka ya kisheria ya RFJ ili watoe tuzo kwa habari katika kategoria nne pana:

  • Ugaidi. Kwa taarifa ambayo:
    • Inapelekea kukamatwa au kutiliwa hatiani kwa yeyote anayepanga, kutenda, kusaidia, au kujaribu vitendo vya kigaidia vya kimataifa dhidi ya Wamarekani au mali ya Marekani ndani ya Marekani au ng’ambo;
    • Inazuia kitendo kama hicho kwanza kisitokee;
    • Inamtambulisha au kutambulisha mahali alipo kiongozi muhimu wa kigaidi;au
    • Inavuruga mifumo ya kifedha ya makundi ya kigaidi ya kigeni. Hii ni pamoja na kuvuruga mifumo mitandao ya utekaji nyara na matukio ya utekaji nyara ambayo yanaunga mkono kifedha mashirika kama hayo.
  • Kuingiliwa kwa Uchaguzi wa Kigeni. Kwa taarifa itakayo:
    • Ongoza utambulisho au eneo la mtu yeyote wa kigeni ambaye kwa makusudi alijihusisha au anajihusisha na uingiliaji kati wa uchaguzi kutoka nje, ikiwa ni pamoja na shughuli inayokiuka shirikisho ya jinai, haki za kupiga kura, au sheria ya fedha ya kampeni, au shughuli kama hiyo ambayo inafanywa na mtu yeyote anayefanya kazi kama wakala wa, au kwa niaba ya, au kwa uratibu na, serikali ya kigeni au biashara ya jinai.
    • Sababisha kuzuiwa, kufadhaika, au utatuzi mzuri wa kitendo cha kuingiliwa kwa uchaguzi wa kigeni.
  • Shughuli Mtandaoni Zenye Nia Mbaya. Kwa taarifa ambayo:
    • Inamtambulisha au kutambulisha mahali alipo mtu yeyote ambaye, kwa maelekezo au chini ya udhibiti wa serikali ya kigeni, anasaidia au kushiriki katika ukiukaji wa Sheria ya Ulaghai na Matumizi Mabaya ya Kompyuta (“CFAA”), 18 U.S.C. § 1030. Hii ni pamoja na kuingilia uchaguzi wa nchi nyingine.
  • Korea Kaskazini. Kwa taarifa ambayo:
    • Inavuruga mifumo ya kifedha ya watu au vyombo husika katika shughuli fulani za kuunga mkono utawala wa Korea Kaskazini, au
    • Inamtambulisha au kutambulisha mahali alipo mtu yeyote ambaye, kwa maelekezo au chini ya udhibiti wa serikali ya Korea Kaskazini anasaidia au kushiriki katika ukiukaji wa Sheria ya Ulaghai na Matumizi Mabaya ya Kompyuta (“CFAA”), 18 U.S.C. § 1030. Hii ni pamoja na mashambulio ya kimtandao na madukizo kwenye mifumo ya serikali ya Marekani.

Kutangaza Ahadi za Tuzo

Mara Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje ameidhinisha kutolewa kwa ahadi ya tuzo, TKM inaitangaza na kushirikiana na hadhira inayolengwa kwa njia inayofaa kitamaduni kwa kutumia vifaa mbalimbali, vikiwemo mitandao ya kijamii, programu za gumzo za kijamii, na vyombo vya habari vya jadi.

Kuchakata Vidokezo

Matangazo ya TKM huwaelekeza watu kutuma ujumbe wa taarifa zao kwa namba za simu za TKM za kupokea vidokezo katika lugha mahususi kupitia programu kadhaa za kutuma ujumbe zinazopatikana na zilizosimbwa, zikiwemo Selo, Telegramu, na WhatsApp. Watu binafsi pia wanaweza kuwasilisha taarifa zao kupitia kwa baruapepe na akaunti za mitandao ya kijamii.TKM husambaza taarifa ya vidokezo inayofaa kwa mashirika mengine ya serikali ya Marekani.

Malipo ya Tuzo

Iwapo taarifa iliyotolewa na kijumbe mtoa habari inaleta matokeo chanya, shirika la serikali ya Marekani linalohusika na uchunguzi wa kesi hiyo linaweza kuamua kumteua mtoa habari huyo kwa malipo ya tuzo. Uteuzi kwa malipo hupitiwa na kamati ya mashirika mbalimbali na halafu kutumwa kwa Waziri kuamua iwapo malipo yatatolewa.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka wa 1984, mpango huu umelipa zaidi ya dola milioni 250 kwa zaidi ya watu 125 duniani kote ambao walitoa taarifa zilioweza kuchukuliwa hatua ambazo zilisaidia kutatua vitisho kwa usalama wa taifa la Marekani.

SUBMIT A TIP

Do Your Part. Secure a Safer World.

There are many ways to submit information to Rewards for Justice.

You may choose from multiple platforms and contact us in numerous languages. To process your information efficiently, we ask you to state your information as succinctly as possible, provide your name, location, and preferred language, and upload all relevant files such as photographs, videos, and documents to support your information. An RFJ representative will soon contact you. Please be patient, as RFJ reads every tip we receive.

Please open your Line app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please open your Viber app to submit a tip. The number is +1 202 702 7843

Please visit our Tor-based tips-reporting channel at: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Wasilisha Kidokezi

Fanya Jukumu Lako - Dhamini Ulimwengu Salama Zaidi

Zipo njia nyingi kuwasilisha kidokezo.

Unaweza kuchagua kutoka majukwaa mengi na kuwasiliana nasi katika lugha nyingi.
Kuchakata taarifa yako kwa ufanisi, tunakuomba kusema taarifa zako kwa maneno mafupi na Dhahiri iwezekanavyo, kutoa jina lako, mahali uliko, na lugha unayopendelea, na kupakia faili zote husika kama vile picha, video, na hati kuunga mkono taarifa yako. Mwakilishi wa TKM atawasliana nawe hivi karibuni. Tafadhali uwe na Subira, kwa kuwa TKM husoma kila kidokezo tunachopokea.

Tafadhali fungua programu yako ya Line ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali fungua programu yako ya Viber ili kuwasilisha kidokezo. Nambari hiyo ni +1 202 718 4649

Tafadhali tembelea idhaa yetu ya kuripotia vidokezo inayotumia mfumo wa TOR katika: he5dybnt7sr6cm32xt77pazmtm65flqy6irivtflruqfc5ep7eiodiad.onion

Skip to content